Mafuriko Dar: Watu 25 wathibitika kufa


image

Mafuriko Dar es Salaam, Tanzania
Watu 25 wamethibitika kufa mkoani
Dar es Salaam nchini Tanzania
kutokana na mvua kubwa
zilizonyesha kwa siku tatu mfululizo
kuanzia Ijumaa hadi Jumapili
iliyopita.
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa
Dar es Salaam, Sadik Meck Sadik
amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo
akisema watu wengine 14
wanadaiwa kufa, lakini
hawajathibitishwa na polisi.
Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es
Salaam wenye wilaya tatu, amesema
watu 11 wamekufa katika wilaya ya
Ilala, huku wengine wawili
hawajaonekana mpaka sasa.
Taarifa kutoka wilaya ya Temeke
imesema watu saba
wamethibitishwa kufa kutokana na
mafuriko yaliyosababishwa na mvua
kubwa iliyonyesha.
Pia kuna taarifa za watu 21 kufariki
dunia katika wilaya ya Kinondoni,
japo hawajathibitishwa.
Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es
Salaam Bwana Sadik amesema
miundombinu ya barabara na
madaraja imeanza kurejeshwa baada
ya kuharibiwa na mafuriko na
kusababisha mkoa wa Dar es Salaam
kukosa mawasiliano ya ndani na pia
kukosa mawasiliano na mikoa jirani.

One thought on “Mafuriko Dar: Watu 25 wathibitika kufa”

Comments are closed.