G7 yazidi kuibana zaidi Urusi


image

Askari wa Ukraine
Viongozi wa nchi Saba tajiri kwa viwanda duniani G7
wamekubaliana kuongeza vikwazo zaidi kwa Urusi
ambapo wamesema imezidi kuifanya Ukraine
isitawalike.
Ikulu ya White House ya Marekani imesema wataanza
kuweka vikwazo hivyo haraka iwezekanavyo kuanzia
siku ya jumatatu na wanatarajia kulenga biashara za
binafsi na ambazo zina uhusiano na Rais Vladimir Putin
wa Urusi.
Viongozi hao wa G7 wameelezea kuguswa kwa na jinsi
Urusi ilivyoshindwa kuacha kuwasaidia wanaoipinga
serikali.
Wametoa wito kwa Urusi kuacha mipango yake kijeshi
ya siri kwenye mpaka na Ukraine.
Kwa upande mwingine viongozi hao wa nchi saba tajiri
duniani wameisifu Ukraine kwa jinsi walivyojizuia kwa
kupanda na wapiganaji waasi.
Serikali ya Ukraine imesema inahofia kuwa Urusi ina
mipango ya kuivamia. Hata hivyo Urusi imesema nchi
za magharibi zina mipango ya kuteka kuitawala nchi
yao.

Godzilla: Bado nina imani na waongozaji wa video wa Tanzania


Rapper Godzilla aka Zizi amesema bado ana imani
kuwa waongozaji wa video wa Tanzania wanaweza
kufanya video nzuri kama wasanii wakijiandaa kwa
nzuri.

image

Amesema anatarajia kumtumia Nick Dizzo kama
muongozaji wa video yake wimbo wake mpya ‘You and
I’ aliomshirikisha Marco Chali ambaye ameutayarisha
pia kupitia MJ Records. “Nick Dizzo ndiye
tuliyempendekeza na Marco,” Zizi ameiambia Bongo5.
“Kwasababu amefanya video kama za akina Izzo B
zimeenda Channel O zinapigwa. Ni kumpa vifaa tu na
kukodisha vifaa vya hela nyingi. Bado naamini wabongo
wana nafasi nzuri kwasababu ukiangalia watu
wanaofanya video nje zinaenda lakini sio zote
zinafanikiwa kupita sehemu wanazotaka. Kwahiyo
inategemea na upepo wa mtu ameangukaje,”
ameongeza.
“Mimi naamini kwenye watu wa ndani sana, mimi
naamini watu wana vitu vingi. Kuna mambo tu Bongo
yanatukwamisha labda kwa system ama vitu fulani
lakini watu wana uwezo mkubwa sana Tanzania.”
source: bongo5